Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), inatangaza bei kikomo za
bidhaa za mafuta ya petroli hapa nchini zitakazotumika
kuanzia Jumatano, tarehe 2
Agosti 2023 saa 6:01 usiku. Kwa mwezi Agosti 2023, bei za
rejareja za mafuta katika
Mikoa ya Dar es Salaam, Tanga na Mtwara ni kama ifuatavyo:
Mabadiliko ya bei za mafuta kwa mwezi Agosti 2023 yanatokana
na changamoto za
upatikanaji wa Dola za Marekani, mabadiliko ya sera za
kikodi, kushuka kwa
thamani ya Shilingi dhidi ya Dola ya Marekani, ongezeko la
gharama za mafuta
katika soko la dunia na gharama za uagizaji wa mafuta. Bei
za mafuta katika miji,
wilaya na mikoa ni kama zinavyooneshwa katika Jedwali Na. 1
na bei za mafuta kwa
wafanyabiashara wa jumla ni kama zinavyooneshwa katika
Jedwali Na. 2.
Wafanyabiashara wa bidhaa za mafuta kwa rejareja wanatakiwa
kuuza mafuta kwa bei
zinazooneshwa katika Jedwali Na. 1. Aidha, wafanyabiashara
wa bidhaa za mafuta kwa
jumla wanatakiwa kuuza mafuta kwa bei zinazooneshwa katika
Jedwali Na. 2. Hatua kali
za kisheria zitachukuliwa dhidi ya mfanyabiashara yoyote
atakayekiuka AGIZO hili.
EWURA inapenda kuwakumbusha wafanyabiashara wa bidhaa za
mafuta kwa jumla na
rejareja pamoja na jamii kuzingatia yafuatayo: -
a) bei kikomo za bidhaa za mafuta ya petroli kwa eneo husika
zinapatikana kupitia
simu za mkononi kwa kupiga namba *152*00# na kisha kufuata
maelekezo.
Huduma hii ni bure na inapatikana kupitia mitandao yote ya
simu za mkononi hapa
nchini.
b) Kwa mujibu wa Sheria ya Mafuta ya mwaka 2015, kifungu
namba 166, bei za
bidhaa za mafuta ya petroli zitaendelea kupangwa na soko.
EWURA itaendelea
kuhamasisha ushindani kwa kutoa taarifa za bei kikomo za
bidhaa za mafuta.
2
c) Kampuni za mafuta ziko huru kuuza bidhaa za mafuta ya
petroli kwa bei ya
ushindani isipokuwa bei hizo zisizidi bei kikomo (Price cap)
au kuwa chini ya
bei iliyoruhusiwa (Floor Price) kama zilivyokokotolewa kwa
mujibu wa Kanuni
za EWURA za Kupanga Bei za Mafuta za Mwaka 2023
zilizotangazwa kupitia
Gazeti la Serikali Na. 421 la tarehe 23 Juni 2023.
d) Vituo vyote vya mafuta vinatakiwa kuchapisha bei za bidhaa
za mafuta katika
mabango yanayoonekana bayana yakionesha bei za mafuta,
punguzo, vivutio vya
kibiashara vinavyotolewa na kituo husika. Pale ambapo
inawezekana kuchagua,
wateja wanashauriwa kununua bidhaa za mafuta katika vituo
vinavyouza mafuta
kwa bei nafuu zaidi ili kushamirisha ushindani. Ni kosa
kuuza mafuta bila kuweka
mabango ya bei inayoonekana vizuri kwa wateja. Adhabu kali
itatolewa kwa
kituo husika kwa kutotekeleza matakwa ya kisheria kwa mujibu
wa kanuni
husika.
e) Wauzaji wa bidhaa za mafuta ya petroli wanatakiwa kutoa
stakabadhi za mauzo
kutoka kwenye Electronic Fiscal Pump Printers (EFPP) na
wanunuzi wahakikishe
wanapata stakabadhi hizo za malipo zinazoonyesha jina la
kituo, tarehe, aina ya
mafuta yaliyonunuliwa na bei kwa lita. Stakabadhi hizo
zitatumika kama kidhibiti
kwa wanunuzi wa mafuta endapo kutajitokeza malalamiko ya
kuuziwa mafuta kwa
bei ya juu kuliko bei kikomo au kuuziwa mafuta yasiyo na
kiwango cha ubora
unaotakiwa. Stakabadhi hizo pia zitasaidia kurahisisha ukusanyaji
wa kodi za
Serikali zitokanazo na mauzo ya bidhaa za mafuta ya petroli.
0 Maoni