Wawekezaji kutoka Urusi wavutiwa na bustani ya wanyamapori Sabasaba

 

Wawekezaji wawili kutoka Urusi wakiambatana na Mwenyekiti wa bodi ya Wakurugenzi ya TAWA Mej. Jen. (Mstaafu) Hamis Semfuko wametembelea banda la Wizara ya Maliasili na Utalii katika maonesho ya 47 ya kimataifa ya kibiashara yanayoendelea Jijini Dar es Salaam na kupata maelezo juu ya fursa za uwekezaji zinazopatikana katika maeneo ya mapori ya akiba na mapori tengefu nchini.

Wawekezaji hao wameipongeza Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kwa juhudi za kuhifadhi Wanyamapori nchini

Kwa nyakati tofauti wakiwa katika bustani ya Wanyamapori hapo jana waliweza kuona Wanyamapori hai mbalimbali kama vile Simba, chui, chatu, mbuni na wengine wengi waliopo katika bustani hiyo na kupongeza juhudi za Serikali katika kuwalinda na kuwahifadhi Wanyama hao kwa ajili ya urithi wa vizazi vijavyo

"Tumetembelea bustani ya Wanyamapori na kuona aina mbalimbali za Wanyama mahali hapa tumefurahi sana, hakika mnatoa viwango vya juu vya huduma Kwa Wanyamapori hawa na tunawaona watu wengi wakifurahi kuwaona Wanyamapori" amesema mmoja wa watalii hao

"Nimependa pia kuona namna mnavyowaleta Wanyamapori karibu na watu wenu Ili waweze kuwaona kirahisi, hii inaonesha tangu utoto watu wenu wanajifunza uhifadhi, hongereni sana na tunawatakia Kila lakheri" ameongeza

Wawekezaji hao wamekuja Nchini Kwa lengo la kutaka kuwekeza katika maeneo mbalimbali yanayosimamiwa na Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA).

Chapisha Maoni

0 Maoni