Watu 44 wafa kwa mlipuko kwenye mkutano Pakistani

 

Watu wapatao 44 wamekufa baada ya kutokea mlipuko nchini Pakistani, wakiwa kwenye mkutano ulioandaliwa na chama cha Kiislam.

Zaidi ya watu 100 pia wamejeruhiwa katika mlipuko huo uliotokea kaskazini-magharibi mwa Wilaya ya Bajaur ambapo chama cha Jamiat Ulema-e-Islam-Fazl (JUI-F) kilifanya mkutano wake.

Polisi wameiambia BBC kwamba wamebaini ushahidi kuwa mlipuko huo ulitokana na mtu anayedaiwa kujilipua kujitoa mhanga.

Zoezi la uokoaji limekamilika na watu wote waliojeruhiwa wamepelekwa hospitali kwa ajili ya kupatiwa matibabu.

Chapisha Maoni

0 Maoni