Ulaya yakabiliwa na joto kali lililoua mtu mmoja Italia

 


Hali ya hewa ya joto imetapakaa katika maeneo ya kusini mwa Ulaya na kaskazini- magharibi mwa Afrika, huku ikitarajiwa kuvunja rekodi ya joto kali katika siku zijazo.

Joto hilo kali linatarajiwa kufikia kipimo cha nyuzi jito 40 katika baadhi ya maeneo ya Hispania, Ufaransa, Ugiriki, Croatia pamoja na Uturuki.

Huko Italia joto litaongezeka na kufikia nyuzi joto 48, ambapo hali ya hatari imetangazwa kwenye miji 10 ikiwamo ya Roma, Bologna na Florence.

Siku ya Jumanne. mwanaume mmoja aliyekwenye umri wa miaka 40 alianguka na kufa kaskazini mwa Italia kutokana na joto kali.

Chapisha Maoni

0 Maoni