Rais wa Iran na Museveni wapinga vitendo vya ushoga

 


Rais wa Iran Ebrahim Raisi amezishutumu nchi za magharibi kuhusiana na misimamo yao ya kukumbatia vitendo vya ushoga, kauli ambayo ameitoa wakati akiwa katika ziara yake nchini Uganda.

Raisi ambaye yupo katika mpango kuimarisha ushirikiano, ikiwa ni safari ya kwanza kwa kiongozi Irani Afrika katika miaka 11, ametoa wito huo akiwa na mwenyeji wake Rais Yoweri Museveni.

"Mataifa ya magharibi yanajaribu kuhamasisha mawazo ya ushoga pamoja na kuhamasisha ushoga, wanajaribu kumaliza kizazi cha binadamu duniani," alisema Rais Raisi.

Rais Museveni alitia saini kuwa sheria muswada wa sheria ya kali ya kupinga ushoga Mei 29, na kuibua kauli za kulalamikiwa na makundi ya haki za binadamu, Umoja wa Mataifa, wanaharakati wa LGBTQ na mataifa ya Magharibi.

Chapisha Maoni

0 Maoni