Mbunge wa Jimbo la Mbarali Wilaya ya Mbarali Mkoani Mbeya Francis Leonard Mtega amefariki leo mchana kwa ajali ya pikipiki pikipiki akiwa anaelekea shambani kwake.
Kwa mujibu wa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Juma Homera, amesema Mtega
amefariki kwa ajali ya pikipiki iliyokuwa imembeba ambayo imegongana na trekta aina
ya power tiller.
Homera amesema mwili wa mbunge huyo umeondolewa katika Hospitali
ya Chimala na kupelekwa Hospitali ya Rujewa ambayo inahuduma la jokofu la
kuhifadhia maiti.
0 Maoni