Chongola azungumzo na Katibu Mkuu wa RPF

 

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Ndugu Daniel Chongolo amekutana na kufanya mazungumza na Katibu Mkuu wa Chama Cha Rwandan Patriotic Front (RPF – Inkotanyi) Ndugu Wellars Gasamagera leo tarehe 1, Julai 2023 katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba Jijini Dar es Salaam.

Katibu Mkuu wa Chama Cha Rwandan Patriotic Front (RPF – Inkotanyi) Mhe. Wellars Gasamagera aliasili nchini usiku wa kuamkia leo, kwa ziara ya siku 5 na kupokelewa na Katibu wa NEC Oganaizesheni Ndugu Issa Haji Ussi Gavu katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere.

Pamoja na mambo mengine Katibu Mkuu wa RPF – Inkontanyi atatembelea kituyo cha televisheni cha Channel 10, mradi wa SGR pamoja na Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere iliyopo Kibaha kwa Mfipa.

Chapisha Maoni

0 Maoni