Ukraine imeanzisha mashambulizi ya kutumia ndege zisizo na
rubani (drone), Moscow, Wizara ya Ulinzi ya Urusi imesema, na kulazimika
kufungwa kwa muda moja wa uwanja mkubwa wa ndege wa nchi hiyo.
Ndege nne zisizo na rubani zimeripotiwa kutumika kufanya
mashambulizi siku ya Jumanne, ambazo pia mashambulizi yake yamelenga eneo kubwa
la Jiji la Moscow.
Wizara ya Ulinzi ya Urusi imesema kwamba ndege zote hizo
zisizo na rubani zimetunguliwa na kuongeza kwamba hazikusababisha majeruhi
yeyote.
Hata hivyo, nchi ya Ukraine haijathibitisha kuhusika na madai
hayo ya Urusi ya mashambulizi.
Baadhi ya ndege zililazimika kubadilishwa muelekeo katika uwanja
wa ndege wa Vnukovo katika kuepusha maafa, ingawa kwa sasa makatazo
yameondolewa.
0 Maoni