Mchezaji Luis Miqissone amerejea tena klabu ya Simba, ikiwa
ni baada ya kutumikia klabu hiyo kwa mafanikio makubwa kabla ya kuuza kwa
miamba ya soka Afrika Al Ahly ya Msiri miaka miwili iliyopita.
Hatua hii inamaliza uvumi wa muda mrefu kuwa mchezaji huyo
atarejea Simba, na leo hii Simba wamemtambulisha rasmi baada ya kufanikiwa
kumsajili kiungo huyo mshambuliaji raia wa Msumbiji kutoka Al Ahly kwa mkataba
wa miaka miwili.
Msemaji wa Klabu ya Simba Ahmed Ally amesema Miquissone
anarejea Simba tena baada ya kuitumikia Simba kwa mafanikio makubwa, kabla ya
kuuzwa kwa miamba ya soka Afrika Al Ahly.
Mchezaji Luis Miqissone amesajiliwa na Simba SC akiwa ni
mchezaji huru, baada ya kuvunja mkataba na timu ya Al Ahly ya Misri.
0 Maoni