Makamu Mwenyekiti wa Chadema Tundu Lissu ameitwa na Ofisi ya
Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jina kutokana na kutoa maneno yasiyo na
staha kumjibu Rais Samia Suluhu Hassan na kusambaa kwenye mitandao ya kijamii.
Kwa mujibu wa nakala ya barua ya wito wa polisi ambayo Lissu
ameiposti kwenye akaunti yake ya twitter maneno hayo ya Lissu yasiyo na staha
kwa Rais Samia yalianza kusambaa mitandaoni kuanzia tarehe 15/07/2023.
Polisi wamesema ili waweze kukamilisha uchunguzi wao, wanamtaka
Lissu afike kwenye Ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jina, Makao
Makuu Madogo ya Dar es Salaam siku ya Alhamisi tarehe 20, Julai 2023 saa 3:00
kamili asubuhi bila kukosa kwa ajili ya mahojiano.
0 Maoni