Jenni Hermoso na Alba Redondo wamefunga magoli mawili wakati
Hispania ikiichakaza Zambia magoli 5-0 katika michuano Fifa ya Kombe la Dunia la
Wanawake.
Kwa ushindi huo Hispania imeionyesha dunia kuwa ni mingoni
mwa timu inayoweza kutwaa kombe hilo, baada ya kutinga hatua ya 16 bora.
Wiki iliyopita Hispania ilianza michuano hiyo katika kundi
C, kwa kupata ushindi rahisi wa magoli 3-0 dhidi ya Costa Rica.
Katika mchezo wa awali hii leo Japan iliichapa Costa Rica
magoli 2-0, na kutinga hatua ya 16 bora ambapo timu hizo sasa zitakutana jumatatu
kuwania kuongoza kundi C.
0 Maoni