Osward Kaijage mwenye umri wa miaka 39 mfanyakazi wa mgodi
wa GGM Geita, anashikiliwa na jeshi la polisi mkoa wa Mwanza kwa tuhuma za
kusababisha vifo vya watu sita na kujeruhi wengine kumi na sita katika ajali
iliyotokea jumamosi wakati watu hao wakifanya mazoezi
Akizungumza na waandishi wa Habari Kamanda wa polisi mkoa wa
Mwanza Wilbroad Mutafungwa amesema Osward amekamatwa katika eneo la kisesa na
bado anahojiwa na jeshi hilo na pindi upelelezi utakapokamilika atafikishwa
mahakamani
Katika hatua nyingine kamanda Mutafungwa ametoa wito kwa
vikundi vyote vinavyofanya mazoezi ya mchakamchaka kujisajiri kwenye ofisi za
utamaduni katika ngazi ya wilaya, manispaa na jiji ili wapate miongozi au
maelekezo ya namna bora ya kufanya mazoezi kwa kuzingatia hali ya usalama wao
na watu wengine
0 Maoni