Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) amesema chama hicho
kitaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo kuboresha
utendaji wa bandari zote za Tanzania kwa kuzingatia maelekezo ya Ilani ya CCM.
Akizungumza jana Jijini Mbeya Katibu Mkuu wa Chama Cha
Mapinduzi (CCM) Taifa Ndugu Daniel Chongolo, amesema kwamba miradi yote
inayotekelezwa na serikali imetokana na misingi ya CCM kutokana na kile
wanachokiamini ili kuleta maendeleo ya taifa.
Ndugu Chongolo amesema kuwa Chama cha Mapinduzi (CCM) kimekuwa
makini katika utekelezaji wa Ilani kwa kuzingatia ahadi za maendeleo ambazo
wamekuwa wakitoa zikiwemo za ujenzi wa barabara.
Katika mkutano huo Ndugu Chongolo amesema, “Bandari zote
zitafanyiwa maboresho ikiwemo ya mkoa wa Tanga, Mtwara pamoja Dar es Salaam
kutokana na kuwa jambo hilo lipo kwenye Ilani ya CCM”.
Amesema kuwa CCM ina malengo na mipango katika kuhakikisha
wanapiga hatua katika kuwaletea maendeleo watanzania, na kuitaka Serikali
kuendelea na mchakato wa awamu ya pili katika makubaliano ya uwekezaji katika
bandari ya Dar es Salaam.
0 Maoni