Kundi la madansa watoto wanaotoka katika mazingira magumu nchini
Uganda, linakaribia kuweka historia, baada ya kutinga fainali ya kipindi cha
vipaji cha Uingereza cha British Got Talent.
Watoto hao wamekuwa wakiwavutia mno majaji pamoja na
mashabiki Uingereza kwa aina ya unenguaji wao na miondoko yao ya kusakata
muziki.
Kundi hilo la Ghetto Kids limekuwa kundi la kwanza kuminyiwa
“golden buzzer” (kitufe cha dhahabu) na moja wa majaji, hata kabla hawajamaliza
shoo.
Kundi ama mtu anayepata kuminyiwa “golden buzzer” hupata
nafasi ya kuingia moja kwa moja hatua ya nusu fainali, hivyo Ghetto Kids
wakatinga hatua hiyo.
Kwa kupata kura nyingi za umma kundi la Ghetto Kids sasa ni
miongoni mwa washiriki 10 ambao watashiriki katika fainali ya British Got
Talent, Jumapili.
Kundi hiyo linaundwa na watoto sita ambao wanaumri wa
kuanzia miaka mitano hadi 13 kutoka katika familia masikini katika Jiji la
Kampala, linalelewa na Dauda Kavuma ambaye ni meneja wao.
0 Maoni