Watu wapatao
40, wengi wao wakiwa ni wanafunzi wameuawa wakiwa shuleni magharibi mwa Uganda,
katika shambulizi lililofanya na waasi wenye uhusiano na kundi la Dola ya
Kiislamu (IS).
Watu wengine
zaidi, wanane wapo mahututi baada ya kufanyika kwa shambulizi hilo kwenye shule
ya sekondari ya Lhubiriha iliyopo Mpondwe nchini Uganda.
Wanafunzi wa
kiume wanaoishi kwenye mabweni ni miongoni mwa waliokufa, huku wengine kadhaa wakiwamo
wanafunzi wakike wametekwa nyara na waasi hao.
Kundi la Allied
Democratic Forces (ADF), lenye maskani yake katika nchi ya Jamhuri ya
Kidemokrasia, limetupiwa lawama kwa kuhusika na shambulizi hilo shuleni.
0 Maoni