Wenyeji wa Euro 2024 Ujerumani, wamefungwa kwa mara ya pili mfululizo, baada ya kukubali kipigo cha mabao 2-0 dhidi ya Colombia nyumbani, katika mchezo wa kirafiki.
Mshambuliaji
wa Liverpool Luis Diaz alifunga kwa kichwa akiunganisha krosi iliyopigwa na Juan
Cuadrado iliyompita Marc-Andre ter Stegen.
Cuadrado aliongeza
goli la pili dakika za mwisho kwa mkwaju wa penati, baada ya Joshua Kimmich aliyetokea
benchi kuunawa mpira.
Ujerumani baada
ya kufungwa 3-2 na Ubelgiji mwezi Machi, walitoa sare 3-3 na Ukraine na
kufungwa 1-0 na Poland mwezi huu.
0 Maoni