Mshambuliaji
wa zamani wa Liverpool Sadio Mane amefunga mara mbili wakati Senegal ikiwachapa Brazil nagoli 4-2 katika mchezo wa kirafiki Lisbon, Ureno.
Kiungo wa
West Ham Lucas Paqueta alikuwa wa kwanza kuipatia Brazil goli katika dakika ya
11 kabla ya Habib Diallo kusawazisha.
Goli la
kujifunga la Marquinhos katika kipindi cha pili liliipatia Senegal goli la
kuongoza huku Mane akiongezea jingine baada ya dakika ya 55.
Marquinhos alifunga
goli la kusawazisha kwa Brazil lakini Mane alifunga goli lake la pili katika
mchezo huo kwa mkwaju wa penati katika dakika za mwisho.
Mchezo huo
uliopigwa katika dimba la Estadio Jose Alvalade wa Sporting Lisbon, ambapo
wachezaji tisa wa Ligi ya uingereza walishuka dimbani.
0 Maoni