Mganga kizimbani kwa kubaka, mauaji na kukata nyeti za mwanamke

 

Watu watatu akiwemo na mganga wa kienyeji aitwaye Ezekiel Charles wamefikishwa Mahakamani kwa kosa la mauaji ya mwanamke aliyejuliakana kwa jina la Esther Lukonu mwenye umri wa miaka 51 wakimtuhumu kujihusisha  na imani za kishirikina

Washtakiwa waliofikishwa Mahakamani ni pamoja na Masunga Mabula mwenye umri wa miaka 32, Ezekiel Charles mwenye umri wa miaka 40 ambae ni mganga wa kienyeji pamoja na Salome Raphael mwenye umri wa miaka 32, ambao wawsomewa kesi namba sita ya mwaka huu mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi Amani Mahimba wa Mahakama ya wilaya ya Magu Jijini Mwanza

Akiwasomea shtaka la mauaji linalowakabili Mwendesha mashtaka wa Serikali mkaguzi Msaidizi wa polisi Chacha Msenye amesema mnamo tarehe kumi ya mwezi watano mwaka huu washtakiwa hao wanadaiwa kumuua mwanamke aitwaye Esther Lukoni kwa kumnyonga shingo kisha wakambaka na kumkata sehemu zake za siri na mwili wake wakautupa kwenye shamba la mihogo.

Mahakama imeelezwa kuwa washtakiwa hao walitenda kosa hilo la mauaji kinyume na kifungu namba 196 na 197 cha sheria ya kanuni ya adhabu sura ya 16 marejeo ya mwaka 2022.

Washtakiwa hao hawakutakiwa kujibu chochote kutokana na Mahakama hiyo kutokuwa na uwezo wa kusikiliza shtaka hilo la mauaji na wamerudishwa rumande katika gereza la wilaya ya Magu hadi tarehe 16 ya mwezi huu kesi hiyo itakapotajwa tena.

Mganga wa kienyeji Ezekiel Charles katikati (mwenye nywele za afro) akiwa amekaa kwenye benchi Mahakamani pamoja na wenzake wawili walioshtakiwa kwa mauaji.


Chapisha Maoni

0 Maoni