Aliyehusika kuwaua watu 2000 Kanisani Rwanda akamatwa

Mmoja wa watu waliokimbia, kati ya watu wanne waliosalia ambao waliohusika na mauaji ya kimbari ya Rwanda amekamatwa, Mwendesha Mashataka wa Mahakama ya Umoja wa Mataifa amesema.

Mtuhuhumiwa huyo Fulgence Kayishema amekamatwa nchini Afrika Kusini siku ya Jumatano, na waendesha mashtaka wameeleza kwamba anatarajiwa kukabiliana na mashataka yake nchini Rwanda.

Kayishema ambaya alikuwa ni afisa wa polisi alishtakiwa mwaka 2001 kuhusiana na tukio hilo, ambalo zaidi ya watu 2000, ambao ni wa kabila la Watusi wanaume, wanawake na watoto waliuawa kwenye kanisa la Katoliki, walipokuwa wamejihifadhi.

Watu wa kabila la Watusi 800,000 waliuawa wakati wa mauaji hayo ya kimbari ya Rwanda 1994, pamoja na Wahutu wenye msimamo wa kati.

Kwa mujibu wa mashtaka Fulgence Kayishema, alihusika moja kwa moja katika kupanga na kutekeleza mauaji ya wakimbizi waliojificha kanisa la Nyange, lililopo Kivumu, Kibuye Aprili 15, mwaka 1994.

Katika mashtaka hayo imeelezwa Kayishema pamoja na wenzake walijaribu kulichoma kanisa lililokuwa na watu walijificha kunusuru maisha yao, na waliposhindwa wakaamua kuwavamia ndani na kuwashambulia kwa mapanga na silaha zingine na kuwaua wote.

CHANZO: BBC

Chapisha Maoni

0 Maoni