Tukio la Ngorongoro kuonesha vivutio
vya utalii mubashara kupitia runings kubwa iliyofungwa katika banda
la Wizara ya Maliasili na Utalii limevutia wananchi wengi
wanaotembelea maonesho ya 50 ya biashara ya kimataifa jijini Dar es
Salaam kwa kuoneshwa maajabu yaliyopo Ngorongoro hususan Kreta ya
Ngorongoro, makundi ya wanyama mbalimbali ikijumuisha pundamilia,
nyumbu, swala, nyati na wanyama adimu kama faru, simba, tembo na na
chui na kujihisi kama wapo nyumbani Ngorongoro.
Afisa
Uhusiano Mkuu wa Ngorongoro Bw. Walter Mairo ameeleza kuwa kupitia
runinga iliyofungwa viwanja vya maonesho wageni wanaotembelea wanaona
wanyama aina mbalimbali ndani ya Kreta, tambarare za Ndutu ambapo
maisha ya Nyumbu kuzaliwa, kukua, kusafiri na kurejea na kuanza
kizazi kipya kila mwaka
Mairo ameongeza kuwa, matukio
mubashara yanaonesha wananchi jinsi teknolojia ya kidigitali na
utalii wa asili vinavyoweza kushirikiana kuelimisha, kuburudisha na
kuonyesha ushahidi kuwa Ngorongoro si tu hifadhi, bali ni jukwaa la
kidunia linalounganisha urithi, biashara na teknolojia sehemu
moja.
Karibu Sabasaba timu yetu yenye wabobezi na watopezi
imejipanga kukupa hadhithi za Ngorongoro zitakazokuduwaza kuwa
Ngorongoro sio mahali pa kuangalia tu, bali mahali pa kuelewa,
kujifunza na kuishi uzoefu usiosahaulika.


0 Maoni