INEC yatangaza majina 115 ya Wabunge wa Viti Maalum

 

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Mhe. Jaji wa Rufani, Jacobs Mwambegele ametangazwa majina ya 115 ya wabunge wa viti maalum, huku chama cha CHAUMMA kikiambulia wabunge wawili wa viti Maalum, CCM ikiwa na wabunge 113.

Jaji Mwambegele ametangaza majina hayo Jijini Dodoma katika kikao cha tume alichokiongoza, kikihudhuriwa na Mhe. Jaji wa Rufaa (Mst) Mbarouk Salim Mbarouk na Katibu wa Tume ambae pia ni Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume, Ramadhani Kailima.

Katika orodha hiyo ya wabunge wa viti maalum 115 waliotangazwa tarehe 7 Novemba 2025 Jaji Mwambegele ametaja majina ya wabunge hao wawili wa viti maalum wa CHAUMMA kuwa ni Devotha Minja na Sigrada Mlingo.

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imesema kwamba inawapongeza wote walioteuliwa kwa nafasi ya Viti Maalum katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.










Chapisha Maoni

0 Maoni