Mamlaka
ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) imepokea kwa masikitiko makubwa
taarifa za kifo cha Dkt. Jane Goodall (1934–2025), mtaalamu mashuhuri wa primatolojia
duniani, mlinzi wa mazingira na mtetezi wa haki za wanyamapori aliyetoa maisha
yake kwa kazi ya kuwalinda.
Kwa
mujibu wa taarifa iliyotolewa na taasisi yake, Dkt. Goodall amefariki dunia Jumatano
akiwa na umri wa miaka 91. Utafiti wake wa muda mrefu kuhusu tabia na maisha ya
sokwe umepanua kwa kiasi kikubwa uelewa wa dunia kuhusu hisia na tabia za
wanyama.
Dkt.
Goodall alijitolea kwa moyo wake wote katika kulinda sokwe na makazi yao ya
asili, jambo lililowavutia na kuwahamasisha vizazi vingi vya wanaharakati wa
uhifadhi kote duniani.
Maisha
yake yamebeba ujumbe wa huruma, maarifa na hatua za dhati katika kulinda sayari
yetu. TAWA inatambua mchango wake wa kipekee na inatoa pole za dhati kwa
familia yake, Taasisi ya Jane Goodall, pamoja na jamii nzima ya wapenda
wanyamapori duniani.
Urithi
wake wa kipekee utaendelea kuwa dira na chachu kwa juhudi za kulinda urithi wa
asili na wanyamapori wa Tanzania kwa vizazi vijavyo.
Pumzika
kwa amani, Dkt. Jane Goodall.

0 Maoni