Kwa mara nyingine kambi maalum ya kupandikiza meno yaanza rasmi Mloganzila

 

Hospitali ya Taifa ya Muhimbili Mloganzila kwa kushirikiana na Daktari Bingwa Mbobezi wa Upasuaji wa Kurekebisha Taya kutoka nchini India, Dkt. Chirag Desai imeanza kambi maalum ya kupandikiza meno kwa watu wenye changamoto ya kupoteza meno kutokana na sababu mbalimbali.

Kupitia kambi hiyo iliyoanza Oktoba 13, 2025 watu zaidi ya 40 watafanyiwa upasuaji wa kupandikiza mzizi wa jino na wengine kupandikizwa meno bandia, kitu kitakachowaweza watu hao kuondokana na hali ya ubogoyo waliyokuwa nayo awali.

Sio mara ya kwanza kwa hospitali hiyo kufanya kambi maalum ya kupandikiza mzizi wa meno na meno bandia kwani kambi hiyo zimekuwa zikifanyika mara kwa mara ambapo kabla ya kufanyika kwa kambi hii watu takribani 67 wameshanufaika na huduma hizo.

Kambi hizi zinatumika kama jukwaa la kubadilishana uzoefu kati ya wataalam kutoka nje ya nchi na watalaam wa ndani ili huduma hizo ziwe endelevu hapa nchini na kuwapunguzia usumbufu wananchi kwenda nje ya nchi kutafuta huduma hizo.

Kambi hiyo ya kupandikiza meno itahitimishwa rasmi Oktoba 17, 2025, ambapo inashauriwa wananchi wenye changamoto ya kupoteza meno kufika hospitalini hapo kwa ajili ya uchunguzi na kupata matibu stahiki.

Chapisha Maoni

0 Maoni