Mchezaji wa mbio za kukimbia kwa ramani kutoka Italia, Mattia Debertolis, amefariki dunia baada ya kupoteza fahamu wakati wa Michezo ya Dunia nchini China wiki iliyopita.
Mwanaume huyo mwenye umri wa miaka 29 alipatikana akiwa hana fahamu na waandaaji wa mashindano hayo siku ya Ijumaa iliyopita wakati wa tukio la orienteering huko Chengdu.
Muitaliano huyo alifariki
siku ya Jumanne, siku nne baada ya kuanguka.
Rais wa Shirikisho la
Kimataifa la Mbio za Ramani (IOF), Tom Hollowell, alisema kuwa "hawezi
kuelezea kwa maneno huzuni kuu isiyopimika kutokana na msiba huu mkubwa."
0 Maoni