Klabu ya Azam FC imehitimisha kwa
mafanikio kambi yao ya mazoezi ya kujiandaa na msimu mpya wa Ligi Kuu Tanzania
Bara, iliyodumu kwa kipindi cha wiki mbili katika mji wa Karatu, mkoani Arusha.
Kambi hiyo, ambayo ilianza mwanzoni
mwa mwezi huu, ilimalizika rasmi siku ya Alhamisi, Agosti 14, 2025, ambapo
benchi la ufundi la timu hiyo linaripotiwa kuridhishwa na hali ya wachezaji,
maadili na viwango vya maandalizi yaliyofikiwa.
Mara baada ya kumalizika kwa kambi
hiyo, kikosi kizima kilipata fursa ya kupumzika kwa muda mfupi kwa kutembelea
Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro, moja ya vivutio maarufu vya utalii nchini,
ambapo wachezaji na benchi la ufundi walipata nafasi ya kufurahia mandhari ya
kuvutia pamoja na wanyamapori waliopo katika hifadhi hiyo ya kipekee.
0 Maoni