Halmashauri ya Muleba yajenga barabara ya Katembe - Mwaloni kwa kiwango cha lami

 

Halmashauri ya Wilaya ya Muleba imefanikiwa kutekeleza mradi wa ujenzi wa barabara ya lami yenye urefu wa zaidi ya kilomita 0.56 katika Kijiji cha Katembe, Kata ya Nyakabango, kwa kutumia fedha za mapato ya ndani kiasi cha Shilingi Milioni 299,608,500.

Mradi huu unasimamiwa na Wakala wa barabara za vijijini na mijini Tanzania (TARURA) huku lengo la mradi huu likiwa  ni kuboresha miundombinu ya barabara kwa ajili ya kurahisisha usafirishaji wa samaki na dagaa ili kuongeza pato la Wilaya na Taifa kwa jumla.

Hadi sasa Mradi huu umefikia 99% za utekelezaji wake na umegharimu kiasi cha Shilingi milioni 299,608,500 huku kazi zilizobakia zikiwa ni  ufungaji wa taa za barabarani na uwekaji wa alama za vivuko vya watembea kwa miguu, ili kuhakikisha usalama na matumizi bora ya barabara hiyo.

Hata hivyo Mradi huu unatarajiwa kunufaisha zaidi ya wakazi 50,000 kutoka katika kata za Mazinga, Ikuza na Nyakabango, pamoja nakunufaisha  wafanyabiashara wa dagaa na samaki kutoka mataifa jirani ya Uganda, Rwanda na Burundi.

Uboreshaji huu wa barabara  unatarajiwa kuchangia kwa kiasi kikubwa pato la Taifa Wilaya na kukuza uchumi wa mwananchi mmoja mmoja.


@tarura_tanzania

@ortamisemi

@kagerayetuofficial 

@kagera_rs

Chapisha Maoni

0 Maoni