Dkt. Biteko ashiriki hafla ya kupokea gawio kutoka kwa mashirika ya umma

 

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko ameshiriki katika hafla ya kupokea gawio na michango kutoka kwa Taasisi, Mashirika ya Umma na Kampuni ambazo Serikali ina hisa zake.

Hafla hiyo imefanyika leo Juni 10, 2025 Ikulu jijini Dar es Salaam na gawio kupokelewa na mgeni rasmi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Akiongea kwa ufupi kabla ya kumkaribisha Rais kuongea, Dkt. Biteko amemshururu Rais Dkt. Samia kwa maono yake yaliyofanikisha siku ya leo Taasisi, Mashirika ya Umma na Kampuni ambazo Serikali ina hisa zake kutoa gawio.


Chapisha Maoni

0 Maoni