TEF apongeza kuzinduliwa Bodi ya Ithibati ya Wanahabari

 

Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) Deodatus Balile amesema uzinduzi wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari ni mwanzo wa kupatikana kwa Baraza Huru la Habari hapa nchini.

Akitoa salamu za TEF wakati wa uzinduizi wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari, Balile amesema kukiwa na Baraza Huru la Habari usimamizi wa kazi za wanahabari utakuwa rahisi, na hata kesi zinazohusu taaluma hiyo zitaamuliwa na Baraza na sio mahakamani tena.

Amesema Baraza Huru la Habari litarahisisha usimamizi wa sekta ya habari na litalinda maslahi ya waandishi wa habari dhidi ya watu wenye nia ovu na sekta hiyo.

Chapisha Maoni

0 Maoni