Mke wa Rais wa Zanzibar, Msarifu na Mwenyekiti wa Bodi ya wadhamini ya Taasisi ya Zanzibar Maisha Bora Foundation (ZMBF), Mhe.Mama Mariam Mwinyi ametoa rai kwa wadau mbalimbali kuwasaidia Watoto na Wazee wenye mahitaji Maalum katika kipindi cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.
Mariam Mwinyi amesema hayo alipovitembelea Vituo vya kuwalea
Watoto SOS, Mazizini na cha Wazee Welezo kuwapa msaada wa vyakula, Mkoa wa Mjini Magharibi tarehe 5 Machi 2025.
Aidha, Mariam Mwinyi ameeleza kuwa ataendelea
kuwasaidia zaidi Watoto na Wazee wenye
mahitaji Maalum ikiwemo vyakula katika kipindi cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani
na Sikukuu ya Eid.
Mariam Mwinyi amewahimiza Watoto kuwa wenye tabia njema na
kufanya ibada katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhani .
Halikadhalika Mama Mariam Mwinyi amewasilisha salamu za
upendo kutoka kwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi
Dkt.Hussein Ali Mwinyi katika vituo hivyo.
Naye, Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Wazee na Watoto Zanzibar Mhe.Dkt.Riziki Pembe Juma amemshukuru Mama Mariam Mwinyi kwa kuendelea kuwajali Watoto wenye mahitaji Maalum katika vituo mbalimbali Zanzibar.





0 Maoni