Rais Samia awaasa Majaji na Mahakimu kutenda haki

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan amewataka majaji na mahakimu wa Mahakama nchini kuhakikisha wanatekeleza wajibu wao kwa mujibu wa makubaliano ya kisheria na kikatiba, na kuwaasa wasijifanye ‘miunguwatu’.

Rais Dkt. Samia ametoa kauli hiyo leo Februari 3, 2025, katika maadhimisho ya Siku ya Sheria yaliyofanyika katika viwanja vya Chinangali Park, Dodoma.

Akifafanua neno la ‘miunguwatu’, Rais Samia akilihusisha na binadamu wanaotekeleza wajibu wao kwa kujipa ukubwa unaofanana na ule wa Mwenyezi Mungu, jambo alilosema watumishi wa taasisi za haki jinai na madai hawapaswi kuwa nalo.

Kazi ya kutoa haki ni kazi ya Mungu, ambayo mbali ya kutoa haki, ana kudra na jaala. Anaweza kuamua akupe au akunyime, alisema Rais Samia na kuongeza sasa hiyo ni kazi ya Mungu.

Kwa upande wake Jaji Mkuu wa Tanzania, Profesa Ibrahim Juma, amesema kuwa migogoro ya ardhi ndiyo chanzo kikuu cha jinai na changamoto nyingi za kijamii na kiuchumi nchini, hivyo inahitaji uangalizi wa hali ya juu katika Dira ya Taifa ya Maendeleo kufikia mwaka 2050.

Jaji Mkuu ameeleza kuwa migogoro ya ardhi inaathiri uwekezaji, biashara, mirathi na masuala mengine ya kijamii.

“Migogoro ya ardhi ni chimbuko la changamoto nyingi. Ikiwa tutaweka mifumo bora ya usimamizi wa ardhi, tutapunguza migogoro mahakamani, na mingi itaishia kwenye usuluhishi,” amesema Prof. Juma.



Chapisha Maoni

0 Maoni