Shirika la Kutetea Haki za Binadamu la Amnesty
International limesema kuwa mwanaharakati na mhariri wa kujitegemea wa Tanzania
Maria Sarungi ametekwa nyara akiwa nchini Kenya.
Katika taarifa kupitia mtandao wa X, shirika la Amnesty
International limesema kwamba Maria alitekwa na wanaume watatu waliokuwa na
silaha na ambao walikuwa na gari nyeusi aina ya Noah.
Taarifa hiyo imeeleza kuwa tukio hilo limetokea majira ya
saa tisa na robo mchana katika eneo la Chaka Place, Mtaa wa Kilimani Jijini Nairobi.
Mkurugenzi Mkuu wa shirika hilo Irungu Houghton ameiambia
BBC kuwa wako katika eneo la tukio wakijaribu kupata taarifa zaidi.
Hii si mara ya kwanza raia wa kigeni kutenkwa nchini
Kenya.
Mwezi Novemba mwaka jana, mwanasiasa wa upinzani wa
Uganda Dkt. Kizza Besigye alitekwa Jijini Nairobi na watu wasiojulikana na
kurejeshwa nyumbani kwao nchini Uganda na kufunguliwa kesi.
Pia, wakimbizi wanne raia wa Uturuki nao walitekwa na
kutimuliwa nchini Kenya kwa lazima na kupelekwa hadi Ankara, ambako
walikabiliwa na tuhuma za kula njama dhidi ya Rais Recep Tayyip Erdogan.
0 Maoni