Serikali na wadau kushirikiana utekelezaji wa afua za elimu ya afya

 

Kaimu Mkurugenzi Msaidizi wa Elimu ya Afya kwa Umma kutoka Wizara ya Afya Dkt. Ona Machangu amesema Serikali itaendelea kushirikiana na wadau katika utekelezaji wa afua mbalimbali za afya.

Dkt. Machangu amebainisha hayo Jijini Dodoma wakati wa kuhitimisha Kikao cha Wadau wanaotekeleza miradi mbalimbali ya afya ikiwemo afua za Elimu ya Afya.

"Tumekuwa na Kikao kizuri sana na tunakuja na Mkakati wa pamoja katika kuhakikisha afua za elimu ya Afya zinatekelezwa kwa ufanisi na upatikanaji wa taarifa na elimu sahihi ya afya, hivyo Serikali itaendelea kushirikiana wadau katika utekelezaji wa afua hizo," amesema.

Beatrice Joseph ni Mratibu wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali yanayotekeleza afua za afya, kutoka Idara ya Sera na Mipango Wizara ya Afya kwa kushirikiana na wadau kuanzia kwenye kupanga hadi utekelezaji.

"Serikali hushirikiana na wadau kuanzia kupanga hadi utekelezaji na lengo ni kuhakikisha afua za afya zinatekelezwa ipasavyo," amesema Beatrice.

Kwa upande wake Mwakilishi wa Mradi wa USAID Afya yangu nyanda za juu Kusini Godfrey Mwanakulya  amesema Kikao hicho kina mchango mkubwa katika utekelezaji wa afua za Elimu ya Afya hasa kwenye masuala ya VVU na UKIMWI.

"Kikao hiki kina umuhimu mkubwa katika utekelezaji wa afua za Afya kama sisi kwenye Mradi wetu unaotekeleza afua za VVU na UKIMWI," amesema.




Chapisha Maoni

0 Maoni