Waliokufa ajali ya ghorofa la Kariakoo wafikia 29

 

Idadi ya vifo vya watu vilivyotokana na kuporomoka kwa jengo la ghorofa eneo la Kariakoo jijini Dar es Salaam imefikiwa 29, baada ya miili mingine tisa kupatikana, wakati zoezi la uokoaji likihitimishwa leo.

Msemaji Mkuu wa Serikali, Thobias Makoba, akizungumza na waandishi wa habari leo akiwa eneo hilo la jengo lilipoporomoka amesema miili hiyo tisa imepatikana wakati shughuli ya kuondoa kifusi ikiendelea.

Makoba ambaye pia ni Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) amesema shughuli ya uokozi imefikia tamati leo siku ya Jumanne Novemba 26, 2024.

Jengo hilo la biashara liliporomoka Jumamosi asuhuhi Novemba 16, 2024 na kusababisha vifo vya watu, majeruhi zaidi ya 80 na uharibifu wa mali zenye thamani ya mamilioni ya fedha.

Chapisha Maoni

0 Maoni