Mwaka 2024 ni mwaka utakaokuwa na joto kali- UN

 

Umoja wa Mataifa (UN) umeonya kuwa mwaka 2024 utakuwa mwaka wenye joto kali katika rekodi duniani, wakati mkutano wake wa mwaka wa hali ya hewa ukianza huko Baku.

Wakuu wa nchi kutoka mataifa 200 wanatarajiwa kushiriki katika wiki mbili zijazo mkutano huo wa COP29 unaofanyika kwenye taifa linalozalishaji mafuta la Azerbaijan.

Msisitizo utawekwa katika kuona ni kwa namba gani nchi zinapanga kutekeleza mpango wa muda mrefu wa kupunguza ongezeko la joto kwa nyuzi joto 1.5, kwa mujibu wa  makubaliano ya Paris 2015.

Chapisha Maoni

0 Maoni