Serikali kupitia Wizara ya Afya kwa Kushirikiana na Ofisi ya Rais ,Tawala za
Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) imetoa nafasi 872 kwa wananchi
watakaowania nafasi ya Wahudumu wa Afya Ngazi ya Jamii katika Halmashauri ya
Wilaya ya Ruangwa Mkoani Lindi ambao watatambuliwa kupitia Mpango Jumuishi wa Wahudumu wa Afya
Ngzi ya Jamii.
Akizungumza katika Kikao na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Ruangwa leo tarehe 9, 2024
katika Ofisi ya Mkurugenzi, Afisa
Mpango wa Taifa wa Wahudumu wa
AfyabNgazi ya Jamii Bi.Orsolina Tolage kutoka Wizara ya Afya, Sehemu ya Elimu
ya Afya kwa Umma amesema kila kitongoji
kutakuwa na Wahudumu wa Afya Ngazi ya Jamii wawili.
"Katika kuhakikisha huduma za Afya zinakuwa karibu zaidi na wananchi Serikali imejipanga ambapo kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa tunatarajia kupata Wahudumu wa Afya Ngazi ya Jamii 872, wawiliwawili kila kitongoji jinsi ya kiume mmoja na jinsi ya kike mmoja , hivyo wataomba nafasi na watachaguliwa kupitia mikutano ya kijiji au mtaa," amesema.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya
ya Ruangwa Frank Chonya ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais
Mhe. Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuweka kipaumbele suala la Afya hasa kwa kuweka Mkakati wa kuwa
na Mpango Jumuishi wa Wahudumu wa Afya Ngazi ya Jamii katika kata 22, vijiji 90 na vitongoji 436 katika Halmashauri hiyo.
"Naishukuru Serikali kwa kuimarisha miradi mbalimbali
ya maendeleo katika katika Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa na hili suala la Mpango Jumuishi wa Wahudumu Ngazi ya Jamii limekuja katika muda
mwafaka hivyo tutashirikiana kuhakikisha uchaguzi wa CHW's unafanyika kwa
ufasaha.
Ikumbukwe kuwa Uchaguzi wa kuwachagua Wahudumu wa Afya Ngazi
ya Jamii katika Halmashauri ya Ruangwa unatarajia kuanza mwezi huu ikiwa ni
katika Utekelezaji wa Mpango Jumuishi wa Wahudumu wa Afya Ngazi ya Jamii
Ulilozinduliwa na Makamu wa Rais Mhe. Dkt. Philip Mpango tarehe
30,Januari,2024 na lengo ni kupata Wahudumu wa Afya Ngazi ya Jamii wapatao
137,294 katika Mikoa yote 26 ya Tanzania Bara ambapo Utekelezaji wa Mpango huo
utafanyika katika kipindi cha miaka mitano kwa awamu .
Katika mwaka wa
kwanza (2023/24) zaidi ya Wahudumu 28,000 watafikiwa na baadaye wastani wa
Wahudumu 27,324 kila mwaka kwa kipindi cha miaka minne mfululizo kuanzia mwaka
2024/25 hadi 2027/28 nchi nzima.
Utekelezaji wa Mpango
huo kwa utaanza katika Mikoa 10 ya
kuanzia ikiwemo Kigoma,Kagera,Tabora
Lindi, Pwani, Tanga, Songwe, Mbeya, Njombe na Geita.
Mpango huo umelenga kusaidia eneo la Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii na kupunguza idadi ya wagonjwa katika vituo vya kutolea huduma za afya kwa kuimarisha huduma za afya kinga pamoja na kuongeza tija na ufanisi katika kutoa huduma za afya kufikia lengo la afya kwa wote.
Na. Elimu ya Afya kwa Umma.
0 Maoni