Zoezi la FTX Ushirikiano IMARA 2024 lafungwa rasmi Rwanda

 

Zoezi la 13 la Medani la Vikundi Vya Ulinzi, Usalama na Taasisi za Kiraia vya Nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (FTX Ushirikiano IMARA 2024) limefungwa rasmi nchini Rwanda leo tarehe 21 Juni 2024.

Akizungumza wakati wa ufungaji wa zoezi hilo, Waziri wa Ulinzi wa Rwanda Mhe. Juvenal Marizamunda amesema kuwa vikundi vyote vilivyoshiriki zoezi hilo vimeonesha weledi mkubwa katika nyanja mbalimbali ikiwemo Ulinzi wa Amani, kukabiliana na majanga ya asili, ugaidi pamoja uharamia.

Naye Kamanda wa vikundi kutoka Jumuiya ya Afrika Mashariki vilivyoshiriki zoezi hilo kutoka JWTZ Brigedia Jenerali Said Hamis Said amesema kuwa vikundi vimeonesha weledi wa hali ya juu katika kutafsiri  na kutekeleza kwa wakati amri na maelekezo mbalimbali yaliyokuwa yakitolewa katika kuwajengea uwezo wa pamoja ili kuviweka tayari pindi vitakapotakiwa kutoa msaada ndani na nje ya Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Kikundi cha Tanzania kimeundwa na JWTZ, Polisi, Uhamiaji, Zimamoto na Uokozi pamoja na Taasisi za Kiraia za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Tukio hilo limehudhuriwa na wageni mbalimbali akiwemo Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) Mheshimiwa Veronica Nduva.




Chapisha Maoni

0 Maoni