Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia
Ackson amesema Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameidhinisha miswada ya sheria
minne iliyopitishwa na wabunge ili iweze kuwa sheria.
Akilitaarifu Bunge la 12, mkutano wa 15 leo Jijini Dodoma,
Spika wa Bunge Dkt. Tulia Ackson amesema katika mkutano wa kumi na nne wabunge
walipitishwa miswada minne ya sheria, ambayo sasa imepata kibali rasmi kwa Rais
Samia ili ianze kutumika kwa mujibu wa sheria.-
Ameitaja miswada hiyo kuwa ni pamoja na Mswada wa Sheria wa
Uchaguzi wa Rais na Madiwani ya mwaka 2023, Mswada wa Sheria ya Tume ya Taifa
ya Uchaguzi 2023, Mswada wa Sheria ya Marekebisho ya Vyama vya Siasa ya mwaka
2023 na Mswada wa Sheria ya Marekebisho mbalimbali ya mwaka 2023.-
“Kwa taarifa hii napenda kulitaarifu bunge hili tukufu kuwa
tayari miswada hiyo minne imeshapata kibali cha Mheshimiwa Rais Dk Samia Suluhu
Hassan na kuwa sheria za nchi,” amesema Spika wa Bunge Dkt. Tulia.-
Kwa sasa sheria hizo zitaitwa: Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani namba 1 ya mwaka 2024, Sheria ya Tume huru ya Taifa ya Uchaguzi namba 2 ya mwaka 2024, Sheria ya Marekebisho ya Sheria za Vyama vya Siasa namba 3 ya mwaka 2024 na Sheria ya Marekebisho mbalimbali ya Sheria namba 4 ya mwaka 2024.
0 Maoni