Rais Dk. Mwinyi aongoza dua kumbukumbu ya Karume

 

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk. Hussein Ali Mwinyi ameongoza kisomo cha Dua na Hitma ya kumuombea Rais wa Kwanza wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Hayati Sheikh Abeid Amani Karume, iliyofanyika Afisi Kuu CCM Kisiwandui  Zanzibar tarehe 07 Aprili 2024.

Viongozi mbalimbali wameshiriki wakiwemo Makamu wa Rais wa Tanzania Dkt. Philip Mpango, Waziri Mkuu wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa, viongozi wengine wa Serikali, Dini , vyombo vya ulinzi na usalama na vyama vya siasa.




Chapisha Maoni

0 Maoni