Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj
Dk. Hussein Ali Mwinyi ameongoza kisomo cha Dua na Hitma ya kumuombea Rais wa
Kwanza wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Hayati Sheikh Abeid
Amani Karume, iliyofanyika Afisi Kuu CCM Kisiwandui Zanzibar tarehe 07 Aprili 2024.
Viongozi mbalimbali wameshiriki wakiwemo Makamu wa Rais wa Tanzania Dkt. Philip Mpango, Waziri Mkuu wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa, viongozi wengine wa Serikali, Dini , vyombo vya ulinzi na usalama na vyama vya siasa.
0 Maoni