Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. Tulia
Ackson na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mhe. Ridhiwani Kikwete
wamewatembelea majeruhi wa ajali ya gari zilizogongana jana tarehe 29 Machi
2024, mabao wamelazwa katika hospitali ya Msoga.
Ajali hiyo ya gari la abiria aina ya Toyota Coaster iliyokuwa
imebeba washabiki wa timu ya Simba waliokuwa wanasafiri toka Mbeya kuelekea Dar
es Salaam kuangalia mpira ambapo gari lao lililigonga lori la mizigo likiingia
barabarani kutoka kupima uzito kwenye mzani maeneo ya Vigwaza.
Akiongea kabla ya kunkaribisha Spika, Mhe. Kikwete ambaye ni
Mbunge wa Chalinze alitoa pole kwa uongozi wa Simba na wafiwa na kuwaombea kwa Mungu
majeruhi wapone na warudi salama Mbeya.
Katika kuonyeshwa kuguswa na tukio hilo pamoja na kutenda
matendo ya huruma, Mbunge huyo aliamua kulipa gharama za huduma za wagonjwa wote
waliohudumiwa hospitalini hapa kwa kutoa fedha kiasi cha shilingi milioni 3.8.
Akizungumza baada ya kumshukuru Mbunge kwa kulipia gharama
hizo, Spika wa Bunge Dk. Tulia alimshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa
uwekezaji mkubwa uliokwisha fanyika hospitalini hapo na kwamba yanayoonekana ni
matundo ya uwekezaji huo.
Pamoja na hayo aliwashukuru wote waliojitotea kusaidia pamoja
na Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Chalinze, na
viongozi wa chama kwa niaba wa wote.
Katika msafara huo wa mashabiki wa Simba 27 walijeruhiwa,
ambapo wote wameruhusiwa isipokuwa wawili ambao watabaki chini ya uangalizi na
wawili walifariki dunia kwa majeraha waliyoyapata katika ajali hiyo.
0 Maoni