Jeshi la Polisi limeanza uchunguzi wa tukio la Mbunge wa
Jimbo la Simanjiro Mhe. Christopher Ole Sendika kushambuliwa kwa risasi akiwa
kwenye gari lake na watu ambao hawajajulikana.
Tukio hilo la mbunge huyo wa CCM kushambuliwa akiwa na dereva
wake limetokea jana Ijumaa, katika kijiji cha Ngabolo wilayani Kiteto mkoa wa
Manyara wakati Mhe. Sendeka akiwa safarini kutokea Dodoma kwenda jimboni kwake
Simanjiro, hata hivyo hawakupata madhara.
Katika taarifa iliyotolewa leo na Msemaji wa Jeshi la Polisi
David Misime amesema Jeshi la Polisi limepokea taarifa za tukio hilo na wanalifuatilia
kwa karibu, ambapo pia uchunguzi wa tukio hilo umeshaanza.
Amesema timu ya wataalamu wa uchunguzi unaohusisha risasi
kutoka Makao Makuu ya Polisi Dodoma, imetumwa kushirikiana na timu ya Mkoa wa
Manyara kuchunguza kwa kina tukio hilo, ili kuwabaini wahusika.
0 Maoni