Mama aliyewanywesha sumu watoto wake naye afariki

 

Mama anayetuhumiwa kuwanywesha sumu watoto wake wawili na kuwasababishia vifo mkoani Mbeya, Dainess Paul Mwashambo (30), amefariki dunia katika hospitali ya mkoa wa Mbeya akipatiwa matibabu.

Taarifa ya Jeshi la Polisi iliyotolewa leo na Kamanda wa Polisi SACP Benjamin Kuzaga mtuhumiwa Dainess amefariki dunia Machi 9, 2024 majira ya saa 10:15 jioni wakati akipatiwa matibabu.

Machi 5, 2024 Dainess akiwa nyumbani kwake Kijiji cha Mashese- Ilungu aliwanywesha sumu ya kuulia magugu aina ya (Pare Force) watoto wake wawili na kusababisha vifo vyao na kisha na yeye alikunywa sumu hiyo iliyopelekea kukimbizwa Hospitali ya mkoa wa Mbeya kwa matibabu.

Taarifa hiyo ya SACP Kuzaga imamalizia kwa kusema kuwa mtuhumiwa Dainess Paul Mwashambo, aliendelea kupatiwa matibabu Hospitalini hapo lakini tarehe 09 Machi, 2024 alifariki duniani.

Chapisha Maoni

0 Maoni