Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amewaonya
Maafisa Manunuzi Mkoani humo wenye tabia ya kuchelewesha taratibu za manunuzi
kwa maslahi yao kuacha tabia hiyo mara moja badala yake kuharakisha taratibu
hizo ili kuleta ufanisi wa shughuli za Serikali ikiwemo kukamilisha miradi ya
maendeleo inayotekelezwa mkoani humo.
Mhe. Malima ametoa onyo hilo wakati wa kikao cha mapitio ya
Bajeti ya Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero ikiwa ni muendelezo wa vikao vya
mapitio ya bajeti za Halmashauri za Mkoa huo kwa mwaka wa fedha 2024/2025.
Mkuu huyo wa Mkoa amebainisha kuwa miradi ya maendeleo mingi
Mkoani humo imekuwa ni viporo moja ya sababu ni ucheleweshwaji wa manunuzi
ambao baadhi yake una walakini kwa maslahi ya mtu binafsi jambo ambalo
amelikemea vikali.
“Yani mtu anakuambia hatujafata taratibu sijui nini huyo ni muongo na dili la kupiga halija kamilika...watu wa kwanza kukanyaga ni hawa maafisa manunuzi,” amesema Mhe. Malima.
0 Maoni