Wakuu wa Umoja wa Mataifa wataka Israel na Hamas kusitisha vita

 

Wakuu wote wa mashirika ya Umoja wa Mataifa, wametoa wito wa kusitishwa mapigano mara moja kwa ajili ya kutoa misaada ya kibinadamu, wakisema kuwa imetosha sasa.

Taarifa hiyo imesema kwa karibu mwezi moja sasa wamekuwa wakishuhudia hali ya kushangaza na kutisha inayojitokeza Israel na maeneo ya Palestina, yakupoteza maisha ya watu kadhaa na mpasuko.

Wakuu hao wa UNICEF, WFP pamoja na Save the Children, wameelezea hali ya kutisha ya vifo vya watu kwa pande zote mbili, na kutaka kuachiwa huru bila ya masharti mateka wa shambulizi la Oktoba 7 wanaoshikiliwa na Hamas.

Naye Waziri wa Mambo ya Nje ya Marekani amewasili nchini Uturuki, akiendelea na ziara ya Kidiplomasia katika ukanda huo, na kutaka kusitishwa kwa mapigano.

Awali akiongea akiwa jijini Baghdad, Antony Blinken alisema kuwa wakuu wa nchi wa ukanda huo wanakaribisha hatua ya kusitishwa mapigano kwa ajili ya misaada ya kibinadamu.

Hata hivyo, Israel imesema kwamba inataka kwanza kuachiwa huru kwa mateka wanaoshikiliwa na Hamas kabla ya kufikiwa hatua ya kusitisha mapigano..

Chapisha Maoni

0 Maoni