Tani 8650 za korosho ghafi zauzwa kwenye mnada wa tatu Lindi

 

Tani 8650 za Korosho ghafi kutoka Chama kikuu cha ushirika RUNALI kinachohudumia wakulima wa Wilaya za Ruangwa, Nachingwea na Liwale Mkoani Lindi zimeuzwa katika mnada wa tatu wa zao hilo kwa bei ya juu ya shilingi 2042 na bei ya chini1950.

Mnada huo umefanyika katika kijiji cha Mkundi kata ya Makata Wilayani Liwale Mkoani Lindi ambapo juma ya makampuni 31 yamejitokeza kununua korosho hizo.

Akiongea kwenye mnada huo Mrajisi wa vyama vya ushirika Mkoa wa Lindi Secilia Sothenes amewataka wakulima kuzingatia ubora wa korosho zao wanazopeleka kwenye maghara.

"Kama tunavyofahamu sasa ni msimu wa mvua umeshaanza hivyo ni vyema wakulima wakahakikisha wanawahi kukusanya korosho zao kutoka shambani sambamba na kuzianika vizuri ili zisiende mnadani zikiwa na unyevu na kupoteza ubora," alisema Sothenes.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama Kikuu cha Ushirika RUNALI amewaahidi wakulima kuendelea kufanya malipo kwa wakati ambapo amesema kuwa mpaka sasa tayari katika minada miwili iliyofanya na chama hiko wakulima wameshalipwa fedha zao.

Chapisha Maoni

0 Maoni