Wakulima waaswa kuacha kuchoma moto mashamba

 

KAMISHNA wa Uhifadhi wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) Prof. Dos Santos Silayo amewataka wananchi hususani wanaojishughulisha na kilimo kuepuka kuchoma moto mashamba na badala yake watumie mbinu mbadala kufuatia hivi karibuni zaidi ya Hekta 500 za Mashamba ya Miti ya Wananchi Wino Halmashauri ya Wilaya ya Madaba kuteketea kwa moto na kujeruhi watu wanne waliokuwa wakizima moto huo.

Kauli hiyo ameitoa leo baada ya kuwatembelea Majeruhi watumishi wanne wa TFS waliojeruhiwa na moto katika eneo la Madaba Kijiji Cha Wino wilayani Songea Mkoa wa Ruvuma waliolazwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili Jijini Dar es Salaam.

Aidha amesema wananchi wanapaswa kujihadhari na uchomaji moto holela katika maeneo ya mashamba sambamba na kuondoa imani potofu za kuchoma moto kunaongeza maisha.

Imeelezwa kwamba Shamba la Serikali la Wakala wa Misitu Wino TFS limeungua kwa sehemu asilimia 0.3

Chapisha Maoni

0 Maoni