Serikali kujaribu suala la biashara na China kwa kutumia shilingi

 

Serikali imelieleza bunge kwamba italifanyia kazi suala la uwezekano wa biashara kati ya China na Tanzania kufanyika kwa kutumia shilingi ya Tanzania.

Kauli hiyo imetolewa leo bungeni Jijini Dodoma, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, wakati wa kujibu swali la Mbunge wa Mafinga Mjini Mh. Cosato David Chumi aliyetaka serikali kuwezesha suala hilo.

Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mh. Hamad H. Chande amesema Serikali italifanyia kazi sula hilo ili kuona nini kinapaswa kufanyika kuwezesha wafanyabishara wa China kukubali matumizi ya sarafu ya Tanzania.

Hata hivyo, Mh. Chande amesema katika biashara ya kimataifa wafanyabiashara wanao uhuru wa kutumia sarafu yoyote inayorahisisha biashara na inayokubalika na nchi nyingine kwa lengo la kupunguza gharama za miamala na muda.

Chapisha Maoni

0 Maoni