Wanasayansi wamesema wamekuta mnyoo wenye urefu wa sentimita 8 ukiwa hai kwenye ubongo wa mwanamke raia wa Australia.
Wanasayansi wamesema tukio hilo ni la mara ya kwanza kutokea
duniani, na kuongeza kwamba huenda mnyoo huo mwekundu ulikuwapo kwenye ubongo
kwa muda wa miezi miwili.
Mnyoo huo ulitolewa kwenye upasuaji kwa mgonjwa huyo
aliyezaliwa Uingereza, na ulikuwa umeathiri mishipa mwembamba ya mbele ya
ubongo.
Watafiti wameonya kwamba tukio hilo lionaonyesha hatari
iliyopo ya kupata maambukizi yanayosambaa kutoka kwa wanyama.
CHANZO: BBC
0 Maoni