Mashujaa wa vita vya Majimaji Nandete waenziwa

 


Wanachi nchini wameimizwa kuwaenzi Mashujaa wa Vita vya Majimaji kwa kudumisha Umoja, Mshikamano, Upendo na Uzalendo kama walivyoishi Mashujaa waliopigania Utu na heshma ya watu wote.

Wito huo umetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Mhe. Christopher Ngubiagai kwaniaba ya Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Mary Masanja, katika Tamasha la Vita vya Majimaji Nandete Kilwa Mkoani Lindi, Vilivyoanzoanzia Nandete Mwaka 1905.

Mhe. Ngubiagai ameongeza kuwa Vita waliopigana Mashujaa wa Vita vya Majimaji dhidi ya Ukoloni, viendelee kuhamasisha na kuongeza nguvu katika Vita dhidi ya Umasikini, watu kufanya kazi Kwa bidii na kwa uwanifu ili nchi hizidi kuinuka kiuchumi.

"Wapiganaji wa vita hivi hawakuwa na silaa za moto bali silaa kubwa walizotumia ni Mshikamano na Upendo usiopimika kwa ajili ya kizazi kilichopita na kizazi hiki, hivyo tuzitumie silaa hizi za Mashujaa wetu katika kuipenda nchi yetu na kudumisha Utamaduni wetu" Mhe. Ngubiagai

Akizungumza kwenye Tamasha hilo, Chifu wa Wamwera Chifu Nakotyo Malibiche Ilulu amesisitiza jamii kudumisha Utamaduni na kuzingatia maadili mema, kupambana na Mmomonyoko wa Maadili unaotokana na vijana kuiga tamaduni za nje zisizofaa.

Naye Chifu wa Kabila la Kimatumbi Mkoa wa Lindi, Mkulungwa Mkulungwa Mbonde Shukuru Mungu ameishukuru Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kuunga Mkono juhudi za Wamatumbi katika uwanzishwaji na undelezwaji wa Tamasha la Vita vya Majimaji jambo linalopelekea wananchi kunufaika na maendeleo mbalimbali hususani ya maboresho ya Miundombinu kama vile barabara.

Na Sixmund Begashe

Chapisha Maoni

0 Maoni