Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar, Mh. Hemed Suleiman Abdullah,
amewataka wahariri wakuu wa vyombo vya habari nchini kutekeleza majukumu ya kuilinda
na kuiendeleza lugha adhimu ya Kiswahili.
Mh. Abdullah ametoa kauli hiyo Zanzibar katika semina ya
Wahariri Wakuu wa Vyombo Vya Habari, iliyolenga namna bora ya kutumia Kiswahili
Sanifu katika Vyombo Habari, katika kuelekea Siku ya Kiswahili Duniani Julai 7.
Amesema kwamba vyombo vya habari vinamchango mkubwa katika kueneza
lugha ya Kiswahili, kutokana kuwa na uwezo wa kuwafikia wananchi wengi, hivyo
ni vyema vikaitumia vizuri lugha hiyo.
“Wengi wenu wanaitumia vizuri lugha ya Kiswahili, ila wapo wachache
wanao kiharibu Kiswahili, ama kwa kutokujua au kwa kutia mbwembwe,” amesema Mh.
Abulallah.
Aidha, Mh. Abdullah amewataka wahariri, kutumia fursa zilizopo
katika vyombo mbalimbali vya habari vya Kimataifa ili kukikuza Kiswahili sanifu
katika ngazi ya kimataifa.
Kwa upande wao Waziri wa Habari, Utamaduni, Vijana na Michezo
Zanzibar Mh. Tabia Mohamed Mwita na Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo
(Bara) Mh. KHamis Mwinyijuma walielezea mikakati mbalimbali inayofanywa katika
kukuza Kiswahili.
Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Utangazaji China,
(CMG) Nairobi Bi. Du Shungfang alitoa wito wa kuandwa kwa umoja wa vyombo vya
habari vinavyotumia lugha ya Kiswahili, ili kuendelea na kuikuza lugha hiyo.
Pia Bi. Du ametaka kusimamiwa ipasavyo mitandao inayofasiri
lugha ya Kiswahili kama ya google ambayo imekuwa na makosa ya kisanifu na
kupotosha watu wanayoitumia ili kufahamu Kiswahili.
Kauli mbiu ya mwaka huu ya Siku ya Kiswahili Duniani,
iliyoanza kuadhimishwa rasmi tangu mwaka 1922, kwa maagizo la UNESCO ni “Kiswahili
Chetu, Umoja Wetu”.
0 Maoni