Watu 150 wamekamatwa
maeneo mbalimbali nchini Ufaransa, kufuatia ghasia zilizotokana na polisi
kumpiga risasi na kumuua dereva kijana wa miaka 17.
Kijana huyo
Mfaransa mwenye asili ya Algeria, Nahel M, alipigwa risasi kwa karibu baada ya
kukataa kusimamishwa na trafiki na kuamuaondoka.
Katika eneo
la Nanterre, ambapo Nahel alipigwa risasi, magari yamechomwa moto na polisi
walifyatua mabomu ya machozi.
Rais wa
Ufaransa Emmanuel Macron aliitisha mkutano wa dharura na kusema ghasia hizo
hazipaswi kuhalalishwa.
0 Maoni